Friday, July 22, 2016

SOMA HII STORI UJIFUNZE KITU

Kijana mmoja alisafiri kwa meli na rafiki zake,
wakiwa katikati ya safari yao meli ilianza
kuzama. Watu wengi pamoja na rafiki wa yule
kijana walikufa maji wakati wanajaribu kujiokoa
kwa kuogelea, lakini yule kijana alifanikiwa
kushika ubao ulioelea majini akaanza kuelea nao,
maji yalimpeleka hadi kisiwa cha mbali sana
ambako hakukuwa na watu wala wanyama
isipokuwa wadudu tu! Alifika ufukweni amechoka
sana na asiyeamini tukio lililotokea, akaishi huko
kwa kula matunda. Aliweza kujenga ka-kibanda
kwa shida sana maana hakuwa na shoka wala
panga, hatimaye akaanza maisha mapya.
Aliishi muda mrefu kisiwani na tayari alishazoea
mazingira yale ya shida japo shida haizoeleki.
Mara zote nyakati za jioni aliwasha moto kwa
kupekecha vijiti. Siku moja kama kawaida yake
aliwasha moto nje karibu na kibanda chake, aliota
moto muda mrefu hatimaye akapitiwa na usingizi.
Alilala hapo hapo hadi usiku wa manane
aliposhtushwa na joto kali lisilo la kawaida.
Kumbe moto ulishika nyasi za kibanda chake na
kibanda chote kikaungua moto.Alilia sana na
kumlaani sana Mungu kwa mateso hayo akisema
"Hivi Mungu nimekukosea nini mpaka unitese
hivi? Pamoja na shida zote hizi bado
unaniongezea shida nyingine, umeteketeza makazi
yangu ilhali nimejenga kwa shida, Hukuridhika
kunitenga mbali na familia yangu nilipoishi kwa
raha? Hukuridhika kuwaua rafiki zangu wote
baharini? Kwanini Mungu umekuwa mkatili hivi?
Bora nife tuu maana nimeshachoshwa na hizi
shida!" akaendelea kulalamika na kumlaani Mungu
hadi kukapambazuka.
Ilipofika asubuhi aliiona meli ikija kwa mbali
kuelekea alipo, alishangaa maana hakuna meli
yoyote inayoweza kwenda kisiwa kile labda kama
imepotea njia. Meli ilipofika ufukweni yule kijana
akaifuata, alienda moja kwa moja hadi kwa
kapteni.Kapteni akamwambia "tuliona moto mkali
sana usiku tukahisi ni meli inawaka moto
tukasema tuje ili tutoe msaada..kwa kweli
tumetembea masaa mengi sana hadi kufika hapa,
mshukuru Mungu maana ametumia moto kutuleta
hapa" yule kijana kusikia hivyo alilia sana,
akajilaumu kwa jinsi alivyo mnung'unikia Mungu.
Akaelewa kuwa Mungu ana njia nyingi za kuleta
msaada kwa mtu. Akapiga magoti akatubu huku
akimshukuru Mungu. Safari ya kurudi nyumbani
ikaanza.
FUNDISHO: Wakati mwingine Kuna mambo
mabaya huwa yanatokea katika maisha yetu
yanayotufanya tuone kama Mungu ametusahau.
Tunamnung'unikia na kumlaumu Mungu bila
kujua kuwa Mungu ana njia nyingi sana kutuletea
msaada. Njia za Mungu huwa zinaonekana kama
ujinga fulani, lakini kiukweli ujinga wa Mungu
ndiyo akili kubwa ya mwisho ya mwanadamu.
Tunasahau kuwa mabaya tunayokutana nayo
yanafanya kazi kwa Manufaa ya hatma zetu.
Unaweza fukuzwa kazi usijue kumbe ndio
unaelekea katika kazi bora zaidi, unaweza
kuachwa na mtu uliyempenda sana ukadhani
ndiyo mwisho wa maisha kumbe Mungu
amekuandalia mtu mwingine mwenye mapenzi ya
dhati mtakayefikia malengo ya kujenga familia,
unaweza kukataliwa na kutengwa na ndugu
kumbe Mungu amekuandalia watu-baki
watakaofanikisha ufikie malengo yako pasipo
masimango ya ndugu, hata rafiki wanaweza
kukusaliti kumbe Mungu amewaondoa makusudi
ili kukuepusha na mabaya waliyoyapanga juu
yako. Sasa usimlaumu Mungu ukadhani
anakuzidishia matatizo, hapo anatafuta njia ya
kuyaondoa hayo matatizo.
Mshukuru Mungu kwa Kila Jambo, kwakuwa
hajawahi kukuwazia mabaya. Anakuwazia mema
sikuzote.
Tafadhari Share kama umeipenda na marafiki
zako wajifunze.

Wednesday, July 13, 2016

MTU SAHIHI WA KUOLEWA AU KUMUOA

USIDANGANYIKE BINTI YANGU..!

Binti mmoja alitaka ushauri kutoka kwa Mwalimu na maongezi yao yalikuwa hivi.. :

🔹Binti : Shallom mwalimu..

🔹Mwl : Shallom maranatha, binti yangu.

🔹Binti : Mwl, kuna swali naomba nikuulize, maana linanisumbua sana kichwa changu.

🔹Mwl : usijal binti yangu, karibu.

🔹Binti : Mwl, mimi ni binti niliyeokoka na nampenda YESU, nina mchumba wangu ninampenda sana na yeye ananipenda pia, lakini yeye hajaokoka. Sasa ninaweza kuwa nae? Tuna malengo ya kuoana.

🔹Mwl : Binti yangu maandiko yanasema,
"Msifungiwe NIRA pamoja na wasioamini (msioane na watu wasiookoka), kwa jinsi isivyo sawasawa. Kwa maana pana Ushirika gani kati ya haki na Uasi? Tena pana shirika gani kati ya Nuru na Giza? Tena pana ulinganifu gani kati ya Kristo na Beliari? Au yeye aaminiye ana sehemu gani pamoja na yeye Asiyeamini? 2 wakorintho 6 :14-16.

Hivi binti yangu, mafuta unaweza ukachanganya na maji na vikakaa pamoja? Ingawa vyote ni vimiminika lakini haviwezi kukaa pamoja. Ni lazima vijitenge, mafuta yatakuwa juu na maji yatakaa chini.

🔹Binti : Lakini Mwl, si anaweza kubadilisha dini?

🔹Mwl : Binti yangu, wokovu si DINI, wokovu ni kuishi maisha matakatifu katika kristo Yesu, wokovu ni KUZALIWA kwa mara ya pili, wokovu ni NEEMA. I Petro 1 : 23, Yohana 3 : 5.

🔹Binti : Basi, Mwl nitamuhubiria aokoke..!

🔹Mwl : Kumuhubiria unaweza binti yangu, lakini sio kumfanya Aokoke, ni Mungu pekee ndiye mwenye uwezo huo. Usidanganyike binti yangu. Tena Yesu aliwaambia hivi Wayahudi :

"Akasema kwa sababu hiyo nimewaambia ya kwamba hakuna mtu Awezaye kuja kwangu (kuokoka) isipokuwa amejaliwa na Baba yangu " Yohana 6 : 65.

🔹Binti : Aah jamani, lakini si kuna andiko linasema mke kama hajaokoka atatakaswa na mumewe kama ameokoka na kama mume ndiye hajaokoka pia atatakaswa na mkewe aliyeokoka?

🔹Mwl : Kweli Mungu alikuwa sawa aliposema watu wangu wanaangamizwa kwa kukosa maarifa (Hosea 4 :6). Binti yangu ni kweli kuna andiko hilo lakini halikuhusu wewe katika mazingira yako ya sasa.

Andiko hilo linawahusu watu waliofunga ndoa kabla hawajaokoka na baadaye mmoja wapo akawa ameokoka, hapo ndipo biblia inashauri kuwa yule aliyeokoka asimuache mwenzake kama atakuwa tayar kuendelea kuwa pamoja, maana yule asiyeokoka hutakaswa kupitia yule aliyeokoka ( 1 wakorintho 7 :12-16).

Hivyo si sawa kwa mtu aliyeokoka kutumia andiko hilo. Binti yangu, Usidanganyike.

🔹Binti : Lakini huyo kijana ananipenda kweli, yaan sijawah ona mwanaume anayenipenda kama yeye, yaan sijaona (kwa kusisitiza).

🔹Mwl : Hahaha, ni kweli binti yangu hakuna mwanaume anayekupenda zaidi yake? Je huyo mwanaume yupo tayar kufa kwa ajili yako? Sidhani binti yangu.

Lakini yupo mwanaume mmoja aliyekubali kufa kwa ajili yako, Yesu pekee ndiye aliyekubali kufa kwa ajili yako hakuna mtu mwingine ANAYEWEZA kufanya hivyo.

Maandiko yanasema : 'Bali alijeruhiwa (Yesu) kwa makosa yetu, Alichubuliwa kwa maovu yetu, Adhabu ya Amani yetu (mimi na wewe) ilikuwa juu yake, Na kwa kupigwa kwake SISI tumepona' the Isaya 53 : 5.

🔹Binti :Lakini Mwl, mi siwez kumuacha yaan ninavyompenda, siwezi jaman.

🔹Mwl : Binti yangu, unawezaje kusema unampenda Yesu ikiwa huwezi kulitii neno lake? Yesu alisema mtu anayempenda hulitii Neno lake (Yohana 14 :23). Na pia alisema mtu asiyekubali kuviacha vitu vyote na kumfuata hawezi kuwa mwanafunzi wake (Luka 14 :33).

🔹Binti :Lakini Mwl, mbona sasa sioni vijana waliokoka wanaonipenda?

🔹Mwl : Binti, mambo ya rohoni hutambulika na kuonekana rohoni. Usitumie akili zako katika hili, ebu mwachie Mungu. 1 Wakorintho 2 : 14.

🔹Binti : Yaani hapa nilipo nimechoka sijui hata nifanyaje.

🔹Mwl : Maandiko yanasema, 'mwenye haki wangu ataishi kwa IMANI, Naye akisita-sita roho yangu haina furaha naye' Waebrania 10 : 38.

🔹Binti : sawa Mwl, nimeelewa.

🔹Mwl :Mungu AKUSAIDIE binti yangu, uwe mtendaji wa Neno na si msikiaji tu. Yakobo 1 : 21.

↪Hivyo ndivyo Maongezi yalivyokuwa kati ya Mwalimu na binti.
..................

Kuna msemo unasema.. :

"USIKUBALI KUMUACHA YESU KWA AJILI YA KITU CHOCHOTE KWA KUWA CHOCHOTE KINAWEZA KUKUACHA WAKATI WOWOTE ILA YESU ATAKUWA NA WEWE WAKATI WOTE KATIKA YOTE "

MUNGU AKUBARIKI..!

Wednesday, April 27, 2011

"Demokrasia sio Ghasia"

      Mataifa mengi ya Afrika    yamejikuta yakiingia katika chuki uhasama uadui hadi vita vya wenyewe kwa wenyewe kutokana na udini ukabila na tofauti za kiitikadi zinazo wapelekea kuzidi kuwa maskini na omba omba kila siku kwa mataifa ya magharibi. 
     Pamoja na hali duni tuliyonayo ya uchumi na teknelojia hafifu bado tunaendelea kuuana sisi kwa sisi  na kuzidi kujirudisha nyuma kimaendeleo kila siku tunagombana sisi tu!
  Pindi tunapata uhuru nchi nyingi za afrika ikiwemo Tanzania tuliongozwa na mfumo wa kisiasa wa chama kimoja (Monoparty) Ila baada ya muda kitambo tulibadili mfumo huo na kuupokea mfumo wa vyama vingi katika siasa, ulopendekezwa na wazungu, 
Nasio kwamba mfumo huo ni mbaya au haufai no!
Ni mfumo mzuri sana wa kuwapa watu fursa zaidi katika kuchagua viongozi wanaowapenda, lengo likiwa ni kuleta changamoto ya utendaji kazi katika serikali kwa ajili ya uongozi bora na maendeleo kwa manufaa yetu sote.    
          Licha ya udhaifu wake Mfumo wa chama kimoja nao ulikuwa na faida kubwa sana kwa watanzania ulitujenga na kutuimarisha kama taifa na undugu miongoni mwetu na kutupa Amani, ushirikiano, upendo na umoja huu uliopo na kudumu hadi leo, Ijapokua ulitubana kidemokrasia kwa kutunyima uwanda mpana katika maamuzi juu ya  serkali inayotuongoza.              
        Kikubwa nachosema ni hiki ; 
                        Watanzania na Afrika nzima kwa ujumla hatuna budi kulitambua hili sisi ni ndugu.
umoja ushirikiano na mshikamano wetu tuliokua nao tusiuharibu!!
kwamba uwepo wa vyama vingi usijenge mgawanyo na makundi miongoni mwetu na kuanza kunyoosheana vidole na kupigana sisi kwa sisi na kuibua matabaka mengine ndani ya taifa moja!
hilo sio lengo.
Leo nchi nyingi za Afrika wanapigana kisa kugombania madaraka , wengine wanadai wanataka demokrasia yaani hawatendewi haki na kuanzisha ghasia na maandamano yanayoondoka na roho za watu wengi! 
ukiwauliza demokrasia jamani demokrasia sio ghasia!!!
mambo yanafanywa kwa mazungumzo na taratibu za kisheria  kisha mabadiliko yanatokea tena kwa amani kabisa na sio kusimaama mbele ya halaiki na kusema kwa hasira na ghadhabu kuwapandia watu chuki na uasi matokeo yake ni kuuana na suluisho lisipatikane!
Serikali sikivu na makini yenye demokrasia ya kweli husikiliza watu wake maana ndio maana ya demokrasia yenyewe kwa kitendo cha serikali kutoridhia maamuzi ya wengi (Majority)  hasa kwa ishu kubwa kama hii ya KATIBA MPYA! ni makosa makubwa hili tutalifananisha na swala la Gadafi kung'ang'ania madaraka pale nchini Libya .Maana kama katiba inanyima haki watu fulani na kuwapenndelea wachache wazidi kutugandamiza maana yake demokrasia hakuna!
         Swala la viongozi wakubwa serikalini kuhujumu serikali na wananchi kwa ujumla alafu wasichukuliwe hatua!  mbaya zaidi wanapambwa na kupewa pango wajifiche pia ni kitendo kibaya na cha kinyama kinachoitia doa serikali na imani ya wananchi kwa serikali kamwe haitapatikana hata kama serikali itavua ngozi yake yote ya mwili , mpaka pale wale wahalifu  wakishughulikiwa kwa hatua madhubuti tena waziwazi kuchukuliwa! 
       Lazima utambue kwamba ukiwa nje ya uwanja ni rahisi sana kulaumu na kumbeza mchezaji anapokosa goli, ukidai ungekua wewe ungeshinda! Pia ni rahisi kuruka ruka na kushangillia mchezaji anaposhinda pasipo kufikiria juhudi na maumivu aliyopata katika kushinda huko! 
      Ni lazima tukubaliane swala la kuongza nchi ni gumu sana, Viongozi wapaswa kuwa na  ushirikiano  katika kila hatua za  utendaji kazi wao serikalini na sio kubezana na kuzodoana kama watoto bungeni! wanabaki kugongagonga benchi wakivinadi vyama vyao wakati sisi wananchi wao tunamaisha magumu!
         Suala la la vyama lisipewe kipaumbele hata kidogo, wakiwa kwenye vikao vya serikali wafanye kazi kwa manufaa ya wananchi wanaowawakilisha.Tanzania bara tuige mfano wa Visiwani jamani!
Lengo ni kupata uongozi bora na sio chama bora, Washauriane na kutoa mapendekezo kwa lengo la kujenga na sio kukosoana! Maana hakuna mkamilifu duniani  kama ni suala la haki au sheria zipo njia nzuri za kuzungumza hadi tukafikia suluhu kuliko kulopoka kwenye halaiki Na kutupandikizia sumu!

         Watanzania sasa tumeamka Tunachagua Kiongozi bora na sio chama!       
         Mwisho namalizia kwa kusema ;-Serikali ya Tanzania kama imechaguliwa na wananchi na itekeleze matakwa ya wananchi wake. 
Viongozi wakiwa serikalini au bungeni waweke itikadi zao za chama na masilahi yao  pembeni.
Na wananchi Tuwe na mtizamo chanya juu ya serikali yetu na Tuache ghasia!   Maana Ghasia sio Demokrasia!          


                                   By S.E.MWITA 
                                                     Profesional Teacher 
                                        contact - phone :+255717010440 
              mail   :P.O.BOX 60080,DSM. 
              email : calmsam1@yahoo.com

Wednesday, April 13, 2011

Literature Review

    
  

Nice Wishes

Full of happiness and joy 
with love, peace and Strength
LET
The
        W Wisdom
        E   Enjoyment
          Encouragement and
        Kisses   from Heaven, surround your days  in this week.

Tuesday, April 12, 2011

Teaching and learning Enviroment!


Teaching and learning environment, 
Affecting much the effectivity of teaching and learning process!

So 
          as to ensure Higher performance in school setting the Government and other organization deals with Education 

must improve these environment of teaching and learning process 


it involve 
            materials such as Desk , Books, Enough buildings for  classrooms, Areas for game and sports and others important materials
      Improve Teaching profession by caring of teachers with enough salaries and provision of well academic prepared teachers from our colleges
              Educational matters to be not elemented with politics!
            
 
              
               
            
IN GOD I TRUST

Friday, April 8, 2011

Fight with target!

 When you Are in this life 
you must have the goals and Aims!
After arranging those aims you have to put some strategies and techniques which will enable you to reach on your goals,    That is what we call instructional objectives which start from general to specific as you break down them and arranging them by budgeting them for each day  to have some thing to do as a fulfillment of your objective and Goals in general!  Never use your time with nothing to gain per each day you have in your life!
             Remember fail to plan is plan to fail!!!! 

 Life is Fighting!  so you must fight harder with targets while knowing where you kick!